Irene Koki Mutungi, anatarajiwa kuwa rubani wa kwanza mwanamke katika bara la Afrika kuidhinishwa kurusha ndege aina ya Boeing 787 Dreamliner.
Bi Mutungi, atairusha ndege hiyo ya Kenya Airways katika safari yake ya kwanza toka Kenya hadi Marekani. Mmoja ya abiria wake atakuwa Rais Uhuru Kenyatta.
